Luke 8:19-21

Mama Yake Yesu Na Ndugu Zake

(Mathayo 12:46-50; Marko 3:31-35)

19 aWakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu. 20 bMtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”

21 cYesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”

Copyright information for SwhNEN